CCCF HUDUMA YA KILA JUMATANO

SEMINA YA VIJANA ILIYOFANYIKA TAREHE 28/06/2015

KIPINDI CHA KWANZA.  
Mwalimu: OCTAVIAN KIYVIRO
SOMOKUTAMBUA KUSUDI LA MUNGU/ KUJUA KUSUDI LA MUNGU.


Matendo 17:11-12”Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wathesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa Moyo,wakayachunguza maandiko kila siku,waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache”.


  •    Tuchunguze maandiko ili tuweze kujua Mungu anazungumza nini kuhusu, Urafiki,Uchumba na ndoa.
             Mithali 25:2”Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo,Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo”


  •       Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo ili sisi tuchunguze.
  •          Inatupasa Kutambua na kujua kusudi la Mungu.
  •         Kuna kusudi au sababu ya Mungu katika sehemu uliyozaliwa.
               Mathayo 1:18-21”Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikua hivi.Mariam mama yake alipokua ameposwa na Yusufu,kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho mtakatifu.Naye Yusufu mumewe kwa vile alikua mtu wa haki,asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.Basi alipokuwa akifikiri hayo,tazama malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu mwana wa daudi usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uwezo wa Roho mtakatifu.Naye atamzaa mwan,  nawe utamwita jina lake Yesu,maana, yeye ndie atakae waokoa watu wake na dhambi zao”.


  •         Kuna sababu za  Mungu kukufanya uwepo duniani.
  •         Inatupasa kutafuta kusudi la Mungu.
 Yeremia  1:4-5”Neno la Bwana lilinijia, kusema kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua,na kabla hujatoka tumboni nalikutakasa,nimekuweka kuwa nabii wa mataifa”


  •         Tutambue Kusudi la Mungu kwanza kwenye Maisha yetu.
               Hekima ya sulemani 7:3-6
  •          Yosefu alitambua kusudi la Mungu
  •          Tutambue Muunganiko wa neno la Mungu na mahusiano.
          Waamuzi 13:1-5”Malaika wa Bwana akamtokea Yule mwanamke akamwambia tazama wewe sasa u tasa huzai,lakini utachukua mimba, nawe utazaa mtoto mwanamume.Basi sasa jihadhari ‘nakuomba usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi, kwani tazama utachukua mimba nawe utamzaa mtoto mwanamume, na wembe usipite juu ya kichwa chake,maana mtoto huyo atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya wafilisti”

               
Mwanzo 1:26-28”Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.Mungu akawabariki , Mungu akawaambia, zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi na kutiisha, mkatawale samaki wa baharini na ndege wa angani,na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”
 Mwanzo 5:2”Mwanamume na mwanamke aliwaumba ,akawabariki akawaita jina lao Adam,siku ile walipoumbwa”
“ Aperson is Soul, Spirit and Body”(Nafsi , Roho na Mwili)
Mwanzo 2:4b-7
Mwanzo 2: 19,20.
=======================================================================
KIPINDI CHA PILI.  
Mwalimu: ROBART MITTI
SOMO:KUJUA KUSUDI LA MUNGU

Matendo 17:10
Waamuzi 13:4”Basi sasa jihadhari, nakuomba usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilichonajisi”
Kusudi la Mungu kwako ni nini?
                Mathayo 1:18-21
                Zaburi 8:3-5 na 6-9


  •          Wewe umefanyika kuwa mwana wa mfalme.
  •          Tusiwatazame Waberoya wakabaki kuwa Waberoya,tuyachunguze maandiko ili tujue kusudi la Mungu katika maisha yetu.
  •          Tunaitwa kuishi kama mfalme.
               Yoshua Bin Sira 23:16-17”Hapo mtakapo livunja agano la Bwana, Mungu wenu alilowaamuru, na kwenda kuitumikia miungu mingine na kujiinamisha mbele yao, ndipo hasira ya Bwana itakopowaka juu yenu, nanyi mtaangamia upesi katika nchi hii njema  aliyowapa”



       


  •   Tusikubali kutikiswa (Unshakable)
  •          Si rahisi kutimiza mapenzi ya Mungu Kama hatutotimiza kusudi la Mungu katika maisha yetu.
               2 Mambo ya Nyakati 7:12-14”Bwana akamtokea sulemani usiku, akamwambia nimesikia uliyoyaomba,na mahali hapa nimejichagulia kuwa nyumba ya dhabihu.Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi,au nikiwapelekea watu wangu tauni.ikiwa watu wangu walioitwa kwa jina langu watajinyenyekesha na kuomba na kunitafuta uso,na kuziacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao,na kuiponya nchi yao”


  •         Tambua nafasi yako kama kijana wa kike na wa kiume utimize kusudi la Mungu kwako.




             KAZI TATU KUU ZA ROHO MTAKATIFU



  •     Kutusaidia kuomba jinsi Mungu anavyotaka tuombe.
  •     Kudhihirisha Matendo makuu ya Mungu.
  •     Roho mtakatifu kudhihirishwa ulimwenguni kwa habari ya dhambi.
Zaburi 32:8”Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea,Nitakushauri jicho langu likikutazama”.
Isaya 30:21” Na masikio yako yatasikia neno nyuma yako,likisema, njia hii,ifuateni mgeukapo kwenda mkono wa kulia na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto”
Mhubiri 4:8…
3 Yohana 1:11-13.