CCCF HUDUMA YA KILA JUMATANO

BIBLIA TAKATIFU

JIFUNZE BIBLIA TAKATIFU


IMANI
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo. - [Warumi 10:17]
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako. - [Mithali 3:5,6]
Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye. - [Marko 9:23]
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. - [2 Wakorintho 5:17]
kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. - [Luka 1:37]
Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate. - [Mathayo 9:29b]
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. - [Waebrania 11:1]
Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku. Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana. Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote. - [Yakobo 1:5-8]
Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao. - [Waebrania 11:6]
Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa. - [Yakobo 2:26]
Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi. - [Warumi 14:23b]
Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. - [Waebrania 10:38]
Tazama, ataniua; sina tumaini; ila hata hivyonitaithibitisha njia yangu mbele yake. - [Ayubu 13:15a]
Nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kutumaini; lakini hamkukubali. - [Isaya 30:15b]
Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe. - [2 Timotheo 2:13]
Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. - [1 Yohana 5:4]
Zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. - [Waefeso 6:16]
Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. - [Mathayo 17:20]
tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. - [Waebrania 12:2]
Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, - [Warumi 5:1]
Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. - [Marko 11:22]
Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali; ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo. Naye mwampenda, ijapokuwa hamkumwona; ambaye ijapokuwa hamwoni sasa, mnamwamini; na kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu, katika kuupokea mwisho wa imani yenu, yaani, wokovu wa roho zenu. - [1 Petro 1:6-9]


UPENDO
Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha. [Kutoka 33:14]
Hata walipokuwa wakishuka mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, Mwambie mtumishi atangulie, (naye akatangulia), bali wewe simama hapa sasa, ili nikuambie neno la Mungu. [1 Samweli 9:27]
Naye akawaambia Yuda, Na tuijenge miji hii, na kuizungushia maboma, na minara, na malango, na makomeo; nchi bado ikalipo mbele yetu, kwa kuwa tumemtafuta Bwana, Mungu wetu; naam, tumemtafuta, naye amemstarehesha pande zote. Basi wakajenga, wakafanikiwa. [2 Mambo ya Nyakati 14:7B]
Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia. [Zaburi 4:4]
Umngoje Bwana, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje Bwana. [Zaburi 27:14]
Ukae kimya mbele za Bwana, Nawe umngojee kwa saburi; Usimkasirikie yeye afanikiwaye katika njia yake, Wala mtu afanyaye hila. [Zaburi 37:7]
Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu. [Zaburi 40:1]
Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi. [Zaburi 46:10A]
Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele. [Zaburi 55:22]
Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; Mungu ndiye kimbilio letu. [Zaburi 62:8]
Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea Katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini. [Isaya 26:3]
Kwa maana Bwana MUNGU, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi, Kwa kurudi na kustarehe mtaokolewa; nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kutumaini; lakini hamkukubali. [Isaya 30:15B]
Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima. [Isaya 32:17]
bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia. [Isaya 40:31]
Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake. [Yeremia 17:7]
Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. [Yeremia 29:11]
Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo. Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu. [Maombolezo 3:25, 26]
Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi. [Mathayo 11:28-30]
Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. [Wafilipi 4:7]
Kwa sababu hiyo nimepatikana na mateso haya, wala sitahayari; kwa maana namjua yeye niliyemwamini, na kusadiki ya kwamba aweza kukilinda kile nilichokiweka amana kwake hata siku ile. [2 Timotheo 1:12B]
huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. [1 Petro 5:7]


FURAHA
Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; Watapiga daima kelele za furaha. Kwa kuwa Wewe unawahifadhi, Walipendao jina lako watakufurahia. [Zaburi 5:11]
Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele. [Zaburi 16:11]
Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha. [Zaburi 30:5]
Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha. [Zaburi 126:5]
Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake. Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema. [Zaburi 128:1, 2]
Na hao waliokombolewa na Bwana watarudi, watafika Sayuni wakiimba; na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia. [Isaya 35:10]
Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe. [Yohana 15:11]
Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu. [Warumi 14:17]