CCCF HUDUMA YA KILA JUMATANO

HUDUMA YA VIJANA ILIYOFANYIKA ST JOSEPH TAR 9/08/2015


Mwalimu: Octavian Kinvyiro
Somo: KUTAMBUA KUSUDI LA MUNGU SIRI NI ROHO MTAKATIFU

Zaburi 32:8. Neno la Mungu linasema; “nitakufundisha na  kukuonyesha njia utakayoiendea, nitakushauri, na jicho langu  likikutazama.”
Roho mtakatifu ni Mungu, na Mungu ni neno. Nisingependa kuingia ndani  zaidi kueleza Roho Mtatifu ni nani, majina yake n.k Lakini  kwa kifupi Biblia inasema Roho mtakatifu ni Mwalimu, msaidizi ,mfariji na majina mengine mengi. Kwa maana hiyo Roho Mtakatifu anauwezo wa kutuonesha kusudi la Mungu kwetu na anatufundisha namna ya kuenenda katika kutimiza kusudi hilo na kutushauri. Mungu ni yeye Yule jana, leo na hata Milele, alichofanya kwa manabii na Mitume hajaacha na wala hataacha kufanya. Anafanya na zaidi kwa njia ya Roho Mtakatifu, tena sisi wa agano jipya ndio zaidi kabisa, Yohane 14: 12, 16: 13,

Je,watu waweza kuongozwa na Roho Mtakatifu ili kujua kusudi la Mungu?

Tulisema ili kuweza kujua kusudu la Mungu, kuna vitu tunaweza kuvitazama au kanuni ambazo tunaweza kuzifuata kama tulivyo ona hapo Mwanzo wa somo.Na kanuni hizo tulizoziona kwanza zaweza kutumika na watu au mtu yoyote atayeamua kukaa na kujichunguza ili kujua nini cha kufanya hapa dunia, bila kujua anatimiza kusudi la Mungu au la!, Kuna watu wametambua vipaji vyao na wanavitumia vyema kabisa. Kwamba wamempa Yesu maisha au la ni kitu kingine, lakini jambo ninaloamini ni kuwa shetani hana uwezo wa kumpa mtu kipaji, zaidi sana anatumia vipaji hivyo hivyo tulivyojaliwa na Mungu kujinufaisha yeye. Kwa hiyo mtu aweza akafuata ndoto zake, anajichunguza anaweza kufanya nini, akafuata msukumo wa ndani na akatimiza lile ambalo ni kusudi la Mungu, hata kama yeye mwenyewe hajui kama hicho ndicho alizaliwa kufanya kwa hapa dunia ili kutimiza fundisho la Katekismu ya kwamba tuliumbwa ili tumpende, tumtumikie na mwisho turudi kwake mbinguni, shetani haumbi, kila mtu aliumbwa na Mungu. Tumpendeje Mungu? Kwa moyo wetu wote, kwa akili zetu  zote na nguvu zetu zote.
Kwa maneno mengine kanuni ya Kufundishwa, kuelekeza na kushauriwa na Roho Mtakatifu ili kujua na kutimiza kusudi la Mungu si kwa wote, bali ni kwa wakristu tu na si wote pia bali wale waliokubali kuongozwa, kufundishwa na kushauriwa na Roho Mtakatifu, kwani katika kutekeleza haya lazima Ushirikiano uwepo kati ya Mfundishaji na mfundishwaji; mshauri na mshauriwa; mwongozaji na mwongozwaji.  (This is two way traffic). Yachunguze maandiko haya kupata nini nichomaanisha:
·        Yohane 3:1-12; 14:15-18; 25- 27; 17:15-22

Kwa maneno kuna vigezo vya kutimiza ili kupata fursa hii ya kuongozwa, kufundishwa, kushauriwa na Mungu.  Na ieleweka hapa hajasema atakufundisha , kukushauiri na kukuongoza katika Kunena kwa Lugha, hapana; kwani Wakristu wengine waliompokea Roho Mtakatifu tunamuwekea mipaka ya kufanya kazi; kunena kwa ndimi au lugha tu basi, na tumewakwanza hata wengine kwa kuwaita hawana Roho Mtakatifu kwa sababu tu hawaneni kwa lugha; si sahihi. Roho Mtakatifu anafundisha na kufunua au kuweka wazi ukweli wa neno la Mungu.
Kanuni ya Kuongozwa na Roho Mtakatifu ni Yetu wapendwa, Tumtumie na tumuulize, tumsikilize. Ngoja nikupe mifano michache toka kwenye biblia ya namna anavyosema na sisi katika kujua kusudi lake kwetu. Kumbuka biblia inasema Mungu ni yeye yule jana, leo na hata milele, AMINA!
·          
Isaya 30: 20- 21; Chunguza neno hilo kama waberoya (Mdo 17: 10-11).
Naomba nikupe home work; Tazama kwa makini maneno yafuatayo;
                                  i.            Walimu wako hawatafichwa tena,
                                ii.            Ila macho yako yatawaona waalimu wako,
                              iii.            Na masikio yako yatasikia neno nyuma likisema, Njia hii ifuate,mgeukapo Kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo Kwenda mkono wa kushoto.

·        Yoel 2: 28; Hata baada ya hayo , ya kwamba nitamimina Roho yangu juu ya wote wenye mwili na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri; wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona MAONO;  sina haja ya kuelezea au kufafanua zaidi, naomba Roho Mtakatifu akufunulie upate ufunuo  (revelation) wa binasfi juu ya neno hili;  Ona, hajasema Baada ya kuwamiminia Roho Mtakatifu wataanza kunena  kwa lugha, nakulia nakupiga kelele; hapana! Soma mwenyewe, na tafuta maana ya neno MAONO au VISION kwa lugha ya Kiingerea.Yaani Wakristu hasa vijana tukimruhusu Roho Mtakatifu atuongoze tutaweza kufanya mambo makubwa yanayooneka (tangible), na kubadilisha ulimwengu huu.

·        1 Nyakati 29: 11-12

·        Mithali 16: 1-3
Haya ni maandiko machache sana, kututhibitishia kuwa Tukikaa sawasawa na Roho Mtakatifu; sky is the limit’ mafanikio ni lazima. Tungeweza kuona mifano mingi ya watu walioshinda kwa kusikiliza na kutii sauti ya Roho mtakatifu twaweza kukesha; Mungu hajabadilika. Mungu wa Ibrahim ndio Mungu wetu, Mungu ya Isaka na Yakobo ndio Mungu wetu, Mungu Petro na Paulo jamani ndio huyo huyo, Mungu wa Papa Yohane wa pili ndio huyo huyo Mungu wetu.
Tutaendelea siku nyingine kujifunza na kuona  vitu au  mambo gani ya kufanya au kutofanya ili kutoa nafasi kwa Roho Mtakatifu kusema na sisi kwa Habari ya kusudi la Mungu.