CCCF HUDUMA YA KILA JUMATANO

SEMINA YA VIJANA ILIYOFANYIKA TAREHE 12/07/2015

           KIPINDI CHA KWANZA. 
Mwalimu: OCTAVIAN KIYVIRO 
SOMO: NAMNA YA KUTAMBUA KUSUDU MUNGU





Kichwa cha habari hapo juu ni mwendelezo wa somo juu ya KUSUDI LA MUNGU katika maisha yetu. Somo lilotangulia tuliyachunguza maandiko (mdo 17:10 - 12) juu ya Kusudi la Mungu kwa kila mmoja.Tuliona mifano mbali mbali ya sababu ya watu Fulani katika biblia ambao kwa uhakika kabisa walijua au walitambulishwa nini kilichowaleta hapa dunia. Mungu hajabadilika ni yeye Yule jana  leo na hata milele.Tuliumbwa kuja kujenga ufalme wa  Mungu hapa dunia.
Kila mmoja ameumbwa kuja kutimiza assignment au jukumu Fulani. Na hili jukumu ni yeye tu  atakaye litimiza  si vyinginevyo.  Ni vyema ikaeleweka kuwa kusudi la Mungu tunalozungumza si kufanya vitu Fulani vya kiroho kama tulivyozoea kwa mfano kuhubiri, kuwa padre au mwijilisti Fulani, ni zaidi ya hapo,Yawezekana mtu akawa ni mkimbiaji, au mchekeshaji,  akawa anatimiza kusudi la Mungu anaweza kuwa mfanyabishara, kuwa mwanasiasa au kufanya kazi Fulani akawa anatimiza kusudi la Mungu.  Kwa neno la Mungu linasema panatofauti ya karama lakini roho ni yeye Yule Yule. Pana tofauti za huduma lakini bwana ni yeye Yule Yule anayehudumiwa.
 Kwa mantiki hiyo ni vyema kijana kabla ya kuwaza kuoa au kolewa akatafuta kwanza nini nilipi kusudi (assignment) la Mungu katika maisha yake. Bila shaka tuliona kwa ufupi  katika somo lililopita kuwa jukumu au kusudi linatangulia ndoa. NDOA SI KUSUDI LAMUNGU BALI NI MPANGO WA MUNGU (Marriage is not a purpose of God, but it is a plan of God). Kipi kinatangulia lengo au mpango mkakati wa kutimiza lengo?


Tuje kwenye somo letu la leo.Utajuaje kusudi la Mungu katika Maishayako.?
Nitakuonyesha njia ambazo Roho mtakatifu amependa kutufundisha kwa namna ya tofauti kabisa,Njia hizo kwa kweli ni practical yaan ni halisia, kama ukizifuata lazima tukutane na assignment yetu toka kwa Mungu. Hakuna short cut/njia ya mkato fuata njia au kanuni lazima ufanikiwe.

  •        Kwanza Mawazo au ndoto zetu za utoto.


Mara nyingi katika umri Fulani hasa kuanzia miaka 8 hadi 12, mtoto anakuwa na mawazo ya kutaka kuwa mtu Fulani au kufanya kitu Fulani.Haya mawazo ni vyema kuyafanyia kazi. Sasa kwa sababu kwa namna moja au nyingine wazazi wengi hawatilii maanani mawazo ya watoto wao katika kipindi hicho,yamkini vijana wengi wanafanya vitu kinyume kabisa na mawazo waliyo kuwa nayo utotoni. Ni vyema ukachunguza mawazo au vitu ulivyotamani kuvifanya ulipo kuwa katika umri huo. Yaweza kuwa hili lilikuwa ni kusudi la Mungu.
Yesu akiwa na umri wa miaka 12 anajua yeye ni mwalimu anawatoroka wazazi wake anaenda kwenye sinagogi na waalimu kwa maana nyingine wenzake,Tayari anajua nini anachopaswa kufanya  au ndoto hizo.
Tusome injili ya luka 2:40-50; Yule mtoto akakua,akaongezeka nguvu,amejaa hekima,na neema ya Mungu ilikuwa juu yake. Basi Wazee wake huenda  Yerusalemu kila mwaka,wakati wa sikukuu ya Pasaka. Na alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili,walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu;na walipokwisha kuzitimiza siku,wakati wa kurudi  kwao,Yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari.Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wakutwa,wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao. Na walipomkosa,wakarejea Yerusalemu hukuwakimtafuta.Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni,ameketi katikati ya waalimu,akiwasikiliza na kuwauliza maswali.Nao wote waliomsikiliza walistaajabu fahamu zake na majibu yake Na walipo mwona walishangaa, na mama yake akamwambia, mwanangu ,mbona umetutenda hivi? Tazama,babayako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.AKAWAAMBIA,kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.

Kumbuka Yesu alikuwa ni  mtu kweli kweli,kwa hiyo yanayofanyika katika somo hapo juu,hakuna Mungu –Yesu ,ni Yesu Mtoto wa miaka 12 mwana Yosefu na Maria. Naomba uyachunguze maandiko uone jinsi ambavyo katika umri huo anajua, anamawazo ya kuwa mwalimu, yupo hekulani anasikiliza na kuuliza maswali kwa waalimu kwa sababu wazazi hawaelekei kuelewa mawazo yake,na ndio maana kuwajibu hawakujua kwamba anapaswa kujifunza ualimu ili kutimiza ndoto zake za kuwa mwalimu walaa hawakuelewa,kama wazazi wengine.  Kuna mambo mengine ya kujifunza kupitia somo (Injilii hapo juu).Lakini kwa ufupi chunguza mawazo aliyokuwa nayo kipindi hicho yanakupa mwanga kujua kusudu la Mungu katika Maisha yetu
  • Tazama au chunguza unawezakufanya nini,kwa maana talanta au kipaji chako


Kila mmoja Mungu amemuumba tofauti na akampa talanta au zawadi au vipaji mbali mbali.Katika kutambua na kuvitumia vipaji tulivyojaliwa na Mwenyezi Mungu, twaweza kujua kusudi la Mungu katika Maisha yetu. Somo Injili ya mathayo 25:14
  •        Chunguza msukumo wa ndani (passion)


Yaani kuna vitu au kitu  au kazi Fulani unatamani kufanya, na msukumo ni mkubwa kabisa toka ndani.  Wakati mwingine unasukumwa  bila kujua sababu. Waweza kuona mtu Fulani anafanya kitu hicho yaani ndani mwako moto unawaka,utamani ingekuwa wewe,waweza kufanya  kama ni kazi hata kwa bure au kwa malipo kidogo kwa jinsi unavyoipenda
  •    Siri ni Roho Mtakatifu


Kwa kweli Roho mtakatifu ndo kila Kitu. Wakristu wengi tunafikiri Roho Mtakatifu ni kwa ajili ya kunena kwa Lugha na mambo mengine kama hayo. Lakini kwa kweli Roho Mtakatifu ni Mwalimu,Kiongozi, Mshauri. Si jambo la ajabu Roho Mtakatifu kutupa wazo la kufanya Biashara Fulani au Kazi Fulani tena ya kuajiliwa  au hata mambo ya siasa na katika hilo tukawa tunatimiza kusudi la Mungu. Naomba nikupe mistari michache    tu na bila shaka tutapata  fursa ya kuingia ndani zaidi katika eneo hili siku tukipata kibali,kwani sehemu hii ndo msingi wa kila kitu katika kutambua kusudi la Mungu.  Zaburi 32;8.  1Mambo ya Nyakati 29:10-14,16-20, Yohani 16:13-15;Mathayo 21:10.
Roho Mtakatifu ni nafsi hai kabisa,anasema,anahisi anaona wivu,n.k.
Tutaingia ndani zaidi kipindi kitakachofuata,ili tujue siri za roho mtakatifu katika maeneo Mengi. Tumshukuru sana Roho Mtakatifu kwa mafunuo yake na mengine mengi mbele yetu. Yohane 16:13-15
========================================================================
KIPINDI CHA PILI. 
Mwalimu: AROBOGAST KANUTI 



Mungu aliwapa Daniel na Yusuph,uwezo wa kupambanua mambo na kupata majibu(solutions) ya vitu.
Tutambue Mungu amechoka theory, Mungu anataka aonekane kwenye maisha yetu,tatizo sisi bado hatujawa tayari (serious), Mungu yeye yupo tayari tangu zamani si sisi tu.
Paulo anamuhisia mtoto wake Timotheo 1timotheo 4:12-16 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo na katika Upendo na imani na Usafi, hata nitakapokuja ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha, Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono na wazee, Uyatafakari hayo ukae katika hayo ili kuendelea kwako kuwe dhairi kwa watu wote, Jitunze nafsi yako na mafundisho yako, Dumu katika mambo hayo maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.

Yoshua 1:1-3, 5-8 “ Ikawa baada ya kufa kwake, Musa mtumishi wa Bwana akamwambia  Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa akasema, Musa mtumishi wangu amekufa,haya basi ondoka, vuka mto huu wa Yordani hata nchi niwapayo wana wa Israeli,Kila mahali zitakapokanyaga nyao za miguu yenu nimewapa ninyi kama nilivyomwapia  Musa tangu Jangwa hili  na mlima huu lebanoni mpaka mto ule mkubwa, mto Frati, nchi yote ya wahiti tena mpaka bahari ile kubwa upande wa machweo ya jua hapo ndipo patakapokuwa mpaka wenu.

Tamani neno la Mungu liwe kweli, tuache hadithi “Yoshua 1:8 “Kitabu hiki cha torati Kisiondoke kinywani mwako, bali yatafaki maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo, maana ndipo utakapoifanikisha njia yako,kisha ndipo utakapositawi sana”


  • Mtu asiudharau ujana wako


Usikubali mtu akaudharau ujana wako tukisoma kitabu cha Walawi na Wafalme tunaona Mungu aliwaita vijana wadogo wa miaka 8,12 na wakaweza kuwa wafalme katika nchi.Tutambue shetani yuko busy Kuvunja hiki kizazi cha vijana wadogo na anajua mbele yako kuna mafanikio(your future is Bright) na amekuwa akiwavunja hata vijana waliookoka.

Kanisa linategemea vijana na nchi inategemea vijana na sisi  ndio wa kuleta mabadiliko. 
1Samweli 17:32-40, 41-46 “Daudi akamwambia Sauli, Asizimie moyo mtu yeyote kwa ajili ya huyu, mimi mtumishi wako nitakwenda kupigana na mfilisti huyu,Sauli akamwambia Daudi huwezi wewe kumwendea mfilisti huyu upigane naye, maana wewe u kijana tu,na huyu ni mtu wa vita tangu ujana wake,Daudi akamwambia Sauli, mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake, na alipokua akija simba au dubu, akamkamata mwana kondoo wa lile kundi mimi hutoka nikamfuata nikampiga,nikamwua, Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia na huyu mfilisti asiyetairiwa atakuwa mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai, Daudi akasema Bwana aliyeniokoa na makucha ya simba na makucha ya Dubu, ataniokoa na mkono ya mfilisti huyu , Sauli akamwambia Daudi enenda na Bwana atakuwa pamoja nawe”.  
Mkaribishe Roho mtakatifu Katika masomo na mitihani yako na Mtu awaye yote asiudharau ujana wako.

  • Tupo ndani ya dunia hii, lakini sisi si wa dunia hii


Tutambue Roho Mtakatifu ni kila kitu na atatupasha mambo ya baadae, maana aliwaonyesha akina Yusuph mambo ya miaka saba ijayo.Tukumbuke Daudi alidharauliwa na Sauli, akadharauliwa na Eliabu kaka yake na Mfilisti pia kwa kuonekana ni kijana mdogo.Roho mtakatifu yupo tayari kutuonyesha mambo makubwa,Kile unachoongea wewe ndicho Mungu atakachotembea nacho, tusidharau neno la Mungu maana halitastawi ndani yetu.Tunatakiwa kuwa mfano na kielelezo siku zote na ufahamu wewe ni chumvi ya ulimwengu.   Tito 2:6-8 “Vivyo hivo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi, katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu”.

Uwe mfano Waefeso 4:29“Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililojema la kumfaa mwenye kuhitaji ili liwape neema wanaosikia” Mungu anataka kukutumia kwenye viwango vya juu, tusitoe maneno maovu bali tuwe faraja kwa wenzetu na wenye shida, Uwe mfano.
Maisha yako kuanzia unapoamka asubuhi mpaka jioni yawe kielelezo na mfano katika mwenendo. Tito 2:8

Lazima uchague kuwa tofauti, usikubali kuenenda na ulimwengu unakoenda,kama kijana, kubali kuwa tofauti ili kuleta mabadiliko.1Petro 4:3-4” Maana wakati wa maisha yenu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya mataifa kuenenda katika ufisadi na tamaa na ulevi,na karamu za ulafi na vileo na ibada ya sanamu isiyo halali, mambo ambayo wao huona ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usiokuwa na kiasi, wakiwatukana”.