CCCF HUDUMA YA KILA JUMATANO

VIJANA WA CCCF WALIPOENDA HOSPITALI YA MUHIMBILI KUWAONA WAGONJWA TAR 15/11/2015


Hawa ni baadhi ya vijana walioenda Kuwaona Wagonjwa Hospitali ya muhimbili

Vijana Wakiwa katika Wodi ya Sewahaji kuwaona Wagonjwa
Vijana Wakiwa pamoja

HUDUMA YA VIJANA ILIYOFANYIKA ST JOSEPH TAR 9/08/2015


Mwalimu: Octavian Kinvyiro
Somo: KUTAMBUA KUSUDI LA MUNGU SIRI NI ROHO MTAKATIFU

Zaburi 32:8. Neno la Mungu linasema; “nitakufundisha na  kukuonyesha njia utakayoiendea, nitakushauri, na jicho langu  likikutazama.”
Roho mtakatifu ni Mungu, na Mungu ni neno. Nisingependa kuingia ndani  zaidi kueleza Roho Mtatifu ni nani, majina yake n.k Lakini  kwa kifupi Biblia inasema Roho mtakatifu ni Mwalimu, msaidizi ,mfariji na majina mengine mengi. Kwa maana hiyo Roho Mtakatifu anauwezo wa kutuonesha kusudi la Mungu kwetu na anatufundisha namna ya kuenenda katika kutimiza kusudi hilo na kutushauri. Mungu ni yeye Yule jana, leo na hata Milele, alichofanya kwa manabii na Mitume hajaacha na wala hataacha kufanya. Anafanya na zaidi kwa njia ya Roho Mtakatifu, tena sisi wa agano jipya ndio zaidi kabisa, Yohane 14: 12, 16: 13,

Je,watu waweza kuongozwa na Roho Mtakatifu ili kujua kusudi la Mungu?

MAFUNGO VIJANA CCCF YALIYOFANYIKA MBAGALA SPIRITUAL CENTRE

MWALIMU ALIYEONGOZA: AROBOGAST KANUTI


MAFUNGO VIJANA CCCF
28-30 AUGUST 2015
MADA
SOMO:    IMANI YA KIJANA MKRISTO KATIKA ULIMWENGU UNAOBADILIKA KWA MUNGU ASIYEBADILIKA
Ulimwengu wetu unabadilika sana, tena kwa kasi kubwa na ya kushangaza sana. Tunajivunia mabadiliko mazuri, lakini pia tunajitahadharisha na mabadiliko mabaya.
Marko 13:31
“Mbingu na Nchi zitapita, lakini Maneno yangu hayatapita kamwe.”
MSIMAMO
Japo dunia na mifumo yake vitabadilika, lakini IMANI zetu kama watu wa Mungu, hazitakiwi kubadilika kamwe.
MABADILIKO HAYA YANATOANA NA NINI?
 Ni mabadiliko yanayotokana na mwingiliano wa jamii mbalimbali kutokana na maendeleo hata kusababisha hizo jamii mbalimbali kuwa kama jamii moja (kijiji)

SEMINA YA VIJANA ILIYOFANYIKA TAREHE 12/07/2015

           KIPINDI CHA KWANZA. 
Mwalimu: OCTAVIAN KIYVIRO 
SOMO: NAMNA YA KUTAMBUA KUSUDU MUNGU





Kichwa cha habari hapo juu ni mwendelezo wa somo juu ya KUSUDI LA MUNGU katika maisha yetu. Somo lilotangulia tuliyachunguza maandiko (mdo 17:10 - 12) juu ya Kusudi la Mungu kwa kila mmoja.Tuliona mifano mbali mbali ya sababu ya watu Fulani katika biblia ambao kwa uhakika kabisa walijua au walitambulishwa nini kilichowaleta hapa dunia. Mungu hajabadilika ni yeye Yule jana  leo na hata milele.Tuliumbwa kuja kujenga ufalme wa  Mungu hapa dunia.
Kila mmoja ameumbwa kuja kutimiza assignment au jukumu Fulani. Na hili jukumu ni yeye tu  atakaye litimiza  si vyinginevyo.  Ni vyema ikaeleweka kuwa kusudi la Mungu tunalozungumza si kufanya vitu Fulani vya kiroho kama tulivyozoea kwa mfano kuhubiri, kuwa padre au mwijilisti Fulani, ni zaidi ya hapo,Yawezekana mtu akawa ni mkimbiaji, au mchekeshaji,  akawa anatimiza kusudi la Mungu anaweza kuwa mfanyabishara, kuwa mwanasiasa au kufanya kazi Fulani akawa anatimiza kusudi la Mungu.  Kwa neno la Mungu linasema panatofauti ya karama lakini roho ni yeye Yule Yule. Pana tofauti za huduma lakini bwana ni yeye Yule Yule anayehudumiwa.
 Kwa mantiki hiyo ni vyema kijana kabla ya kuwaza kuoa au kolewa akatafuta kwanza nini nilipi kusudi (assignment) la Mungu katika maisha yake. Bila shaka tuliona kwa ufupi  katika somo lililopita kuwa jukumu au kusudi linatangulia ndoa. NDOA SI KUSUDI LAMUNGU BALI NI MPANGO WA MUNGU (Marriage is not a purpose of God, but it is a plan of God). Kipi kinatangulia lengo au mpango mkakati wa kutimiza lengo?


SEMINA YA VIJANA ILIYOFANYIKA TAREHE 28/06/2015

KIPINDI CHA KWANZA.  
Mwalimu: OCTAVIAN KIYVIRO
SOMOKUTAMBUA KUSUDI LA MUNGU/ KUJUA KUSUDI LA MUNGU.


Matendo 17:11-12”Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wathesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa Moyo,wakayachunguza maandiko kila siku,waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache”.


  •    Tuchunguze maandiko ili tuweze kujua Mungu anazungumza nini kuhusu, Urafiki,Uchumba na ndoa.
             Mithali 25:2”Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo,Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo”


  •       Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo ili sisi tuchunguze.
  •          Inatupasa Kutambua na kujua kusudi la Mungu.
  •         Kuna kusudi au sababu ya Mungu katika sehemu uliyozaliwa.
               Mathayo 1:18-21”Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikua hivi.Mariam mama yake alipokua ameposwa na Yusufu,kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho mtakatifu.Naye Yusufu mumewe kwa vile alikua mtu wa haki,asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.Basi alipokuwa akifikiri hayo,tazama malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu mwana wa daudi usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uwezo wa Roho mtakatifu.Naye atamzaa mwan,  nawe utamwita jina lake Yesu,maana, yeye ndie atakae waokoa watu wake na dhambi zao”.


  •         Kuna sababu za  Mungu kukufanya uwepo duniani.
  •         Inatupasa kutafuta kusudi la Mungu.
 Yeremia  1:4-5”Neno la Bwana lilinijia, kusema kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua,na kabla hujatoka tumboni nalikutakasa,nimekuweka kuwa nabii wa mataifa”


  •         Tutambue Kusudi la Mungu kwanza kwenye Maisha yetu.
               Hekima ya sulemani 7:3-6
  •          Yosefu alitambua kusudi la Mungu
  •          Tutambue Muunganiko wa neno la Mungu na mahusiano.
          Waamuzi 13:1-5”Malaika wa Bwana akamtokea Yule mwanamke akamwambia tazama wewe sasa u tasa huzai,lakini utachukua mimba, nawe utazaa mtoto mwanamume.Basi sasa jihadhari ‘nakuomba usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi, kwani tazama utachukua mimba nawe utamzaa mtoto mwanamume, na wembe usipite juu ya kichwa chake,maana mtoto huyo atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya wafilisti”

               

HUDUMA YA VIJANA JUMAPILI YA TAREHE 14/6/2015

SOMO:KIJANA ANATAKIWA AWE NA SIFA ZA UFALME
MWALIMU: STELLA MITTI
a)Wewe kama kijana lazima uwakilishe ufalme,uwe mtoto wa mfalme
b) Lazima uwe na Imani kama mfalme,kwamba ufalme upo.(Mathayo 12:28 , Luka 17:21-25)
Kwenye ufalme lazima kuwe na uvumilivu na matumaini.
c) Ufalme wa Mungu  hauyumbishwi( Unshakable).(waebrania 12:28)
     WEWE NI MTOTO WA MFALME

                           Mwalimu Stella Mitti akiwa na Vijana kwenye semina